Swahili   |   English
Ufilisi watu Binafsi

Ombi la mdaiwa

  • Mdaiwa atawasilisha taarifa kuhusu mali zake Mpokeaji Rasmi kabla ya kufungua Ombi mahakamani.
  • Mpokeaji Rasmi atatoa hati ya kukiri kupokea na kuiwakilisha Mahakamani.
  • Mahakama ikiridhika itatoa amri ya Upokeaji na Mpokeaji Rasmi anakuwa Mpokeaji aliyeteuliwa.
  • Mpokeaji Rasmi ataendelea chini yaSheria ya Ufilisi, Sura ya 25 Toleo la 2002 na kufilisi mali ya mdaiwa.


Ombi la Mdai

  • Mdai atafungua ombi mahakamani kupata amri ya kufilisi mali ya mdaiwa.
  • Mpokeaji Rasmi atatoa hati na kuwasilisha mahakamani.
  • Mahakama itatoa amri ya Upokeaji na Mpokeaji Rasmi anateuliwa kuwa Mpokeaji.
  • Mpokeaji Rasmi ataendelea chini ya Sheria ya Ufilisi, Sura ya 25 toleo la 2002 na Kanuni zake kufilisi mali ya mdaiwa.