RITA
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
Registration Insolvency and Trusteeship Agency
MEDIA CENTRE
March
13
2025
MKUTANO WA WAJUMBE WA BODI ZA WADHAMINI
News & Update
JAFARI MALEMA
`

Waziri wa Sheria na Katiba, Dkt. Damas Ndumbaro amewaonya baadhi ya viongozi wa Bodi za wadhamini wa taasisi za kidini, vyama vya siasa na vyama vya michezo kwa ubadhirifu na matumizi mabaya na kujimilikisha mali za taasisi hizo kinyume na sheria.

Hayo ameyasema leo Machi 13, 2025 wakati wa mkutano wa wajumbe wa bodi za wadhamini zilizomo Mkoa wa Dar es Salaam uliofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere.

“Sisi sote ni mashahidi wa ongezeko la migogoro katika taasisi mbalimbali nchini ambayo inasababishwa na mapungufu ya usimamizi wa majukumu ya bodi za wadhamini. Inashangaza kuona hali hii inajitokeza hata katika taasisi za kidini ambazo kikawaida zinatakiwa kuwa mfano wa kuigwa katika jamii,” amesema Dkt. Ndumbaro.

Pia, amebainisha kuwa, migogoro katika taasisi na jamii inatokana na baadhi ya wadhamini kufuja fedha na kutumia hovyo mali za taasisi hususani ubadhirifu wa fedha.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wizara kwa RITA Dkt. Amina Msengwa amewataka wajumbe wa bodi za wadhamini kuheshimu Sheria na katiba zao kwani zimebainisha ukomo wa uongozi wao, ufanyaji wa maamuzi na usimamizi wa mali za taasisi na kutambua kuwa wao siyo wamiliki wa mali hizo bali ni wasimamizi tu.

Naye Kabidhi Wasii Mkuu na Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA Bw. Frank Kanyusi amesema kuwa kikao hicho ni muendelezo wa mikakati yao ya kukutana na wadau ili kwa pamoja waweze kutatua changamoto za uendeshaji na usimamizi wa mali za waumini au wanachama wao kwa maslahi mapana ya jamii na Taifa kwa ujumla.

Tags : #Insolvency