RITA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro leo Aprili 24, 2025 amekutana na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo pamoja na Mwakilishi wa Mhimili wa Mahakama kwa ajili ya maandalizi kuelekea uwasilishaji wa makadirio ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025 - 2026.
Kwa upande wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) Kabidhi Wasii Mkuu na Afisa Mtendaji Mkuu Bw. Frank Kanyusi ameahiriki katika kikao hicho na amewasilisha makadirio na vipaumbele vya bajeti ya Wakala kwa mwaka wa fedha 2025/2026.